Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli na Rais wa Jamhuri ya Msumbiji na Mwenyekiti wa SADC Mhe. Filipe Jacinto Nyusi wakipunga mkono kuwaaga wananchi waliojitokeza wakati wa kuweka jiwe la msingi ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda -Chato mkoani Geita
Rais wa Jamhuri ya Msumbiji, Mhe. Filipe Jacinto Nyusi leo tarehe 11 Januari, 2021 amefanya ziara ya kikazi ya siku 1 hapa nchini ambapo amekutana na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli katika Wilaya ya Chato Mkoani Geita.