Amiri Jeshi Mkuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwapungia mikono wananchi waliofurika katika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam katika Maadhimisho ya sherehe za miaka 53 ya Uhuru wa Tanzania Bara akiwa katika Gari maalum liliozunguuka katika uwanja huo leo.Kushoto ni Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama,Jenerali Davis Mwamunyange.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Vyombo vya Ulinzi na usalama Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete pamoja na Viongozi wa Kitaifa wakisimama wakati wimbo wa Taifa ukipigwa katika kilele cha sherehe za maadhimisho ya miaka 53 ya Uhuru wa Tanzania Bara zilizofanyika leo katika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam
Amiri Jeshi Mkuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete Pamoja na Rais wa serikali ya mapinduzi ya Zanzibar wakiaangalia kwa makini gwaride lililoandaliwa rasmi na Vyombo vya Ulinzi na Usalama kwa ajili ya Maadhimisho ya miaka 53 ya Uhuru katika Uwanja wa Uhuru Desemba 09, 2014 Jijini Dar es salaam
Amiri Jeshi Mkuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akikagua gwaride lililoandaliwa rasmi na Vyombo vya Ulinzi na Usalama kwa ajili ya Maadhimisho ya miaka 53 ya Uhuru katika Uwanja wa Uhuru Desemba 09, 2014 Jijini Dar es salaam
Vikosi vya Ulinzi na Usalama vikipita mbele ya Amiri Jeshi Mkuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete kwa ukakamavu wakati wa maadhimisho ya miaka 53 ya Uhuru katika Uwanja wa Uhuru Desemba 09, 2014 Jijini Dar es salaam
Sehemu ya viongozi na wananchi waliofika katika Uwanja wa Uhuru Desemba 09, 2014 Jijini Dar es salaam kushuhudia maadhimisho ya sherehe za miaka 53 ya Uhuru wa Tanzania