Monthly Archives: October 2015

RAIS DKT. JAKAYA MRISHO KIKWETE APOKEA HATI ZA UTAMBULISHO KUTOKA KWA MABALOZI WANE OKTOBA 28, 2015

 Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete Oktoba 28,2015 amepokea hati za utambulisho kutoka kwa mabalozi wanne wanaziwakilisha nchi zao hapa Tanzania.Mabalozi waliowasilisha hati zao kwa Rais Kikwete Ikulu  ni pamoja Mhe.Yasser Ahmed Al Eldin Elshawaf Balozi mpya wa Misri hapa nchini, Mhe.Yahel Vilan Balozi mpya wa Israel nchini Tanzania, Mhe.Bayani Mangibin balozi mpya wa Ufilipino nchini na Mhe. Tan Puay Hiang Balozi mpya wa Singapore nchini Tanzania.   Pichani Mabalozi hao wakiwasilisha hati zao za utambulisho.

1 Balozi mpya wa Misri hapa nchini Mhe.Yasser Ahmed Al Eldin Elshawaf wakiwalisha hati zake za utambulisho kwa Rais Kikwete Ikulu jijini Dar Es Salam  

2 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akipokea hati za utambusho kutoka kwa Mhe.Yahel Vilan Balozi mpya wa Israel hapa nchini

3 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akipokea hati za utambulisho kutoka kwa mhe.Bayani Mangibin Balozi mpya wa Ufilipino nchini Tanzania. 

4Balozi mpya wa Singapore nchini Tanzania Mhe.Tan Puay Hiang akiwasilisha hati zake za utambulisho kwa Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete ikulu jijini Dar es salaam 

RAIS KIKWETE AKABIDHI VITABU CHUO CHA ULINZI CHA TAIFA (NATIONAL DEFENCE COLLEGE) OKTOBA 26,2015

1mnmhhAmiri Jeshi Mkuu Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Davis Mwamunyange vitabu kwaajili ya Chuo Cha ulinzi cha Taifa National Defence College (NDC) katika hafla fupi iliyofanyika ikulu jijini Dar es Salaam,Kulia ni Mkuu wa Chuo hicho cha NDC Meja Jenerali Gaudence Milanzi. 

2Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue,Mkuu wa Majeshi ya ulinzi Jenerali Davis Mwamunyange,Mkuu wa Chuo Cha NDC Meja Jenerali Gaudence Milanzi wakiangali baadhi ya vitabu ambavyo Rais ameviakbidhi kwaajili ya matumizi ya Chuo hicho.  

3Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete,Katibu mkuu kiongozi Balozi Ombeni Sefue(watatu kushoto),Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Davis Mwamunyange,(kushoto) na Mkuu wa Chuo cha Ulinzi Cha Taifa(NDC) Meja Jenerali Gaudence Milanzi(kulia) wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi waandamizi wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania muda mfupi baada ya Rais Kikwete kukabidhi vitabu kwaajili ya National Defence College) katika hafla iliyofanyika ikulu jijijini Dar es Salaam