Daily Archives: September 1, 2016

RAIS DKT. JOHN POMBE MAGUFULI AZUNGUMZA NA WAHANDISI, AMUAPISHA KATIBU MKUU WA WIZARA YA FEDHA PIA AWAPONGEZA JWTZ KWA KUTIMIZA MIAKA 52 TANGU KUANZISHWA KWAKE LEO SEPTEMBA 1,2016

1..Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Doto James kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango.

2Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi wakiwa katika picha ya pamoja na Katibu Mkuu mteule wa Fedha na Mipango Doto James mara baada ya kuapishwa.

3

 

4Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Wahandisi mbalimbali wa ndani na nje ya nchi kabla ya kufungua rasmi Maadhimisho ya 14 ya Siku ya Wahandisi kwa mwaka 2016.

6

 

7Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipewa maelezo na Kanali Erick Mhoro kuhusu sifa tabia na uwezo wa Ndege vita wakati wa kilele cha Maadhimisho ya miaka 52 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania JWTZ zilizofanyika katika Kikosi cha Usafirishaji wa anga (Air Wing) Ukonga jijini Dar es Salaam.

8 Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania Jeneral Davis Mwamunyange akiwa pamoja na Maafisa na askari wakimpigia makofi Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt. John Pombe Magufuli wakati akizungumza katika kilele cha kilele cha Maadhimisho ya miaka 52 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania JWTZ katika Kikosi cha Usafirishaji wa anga (Air Wing) Ukonga jijini Dar es Salaam.

10Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia jambo na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania Jeneral Davis Mwamunyange mara baada ya kuzungumza na Maafisa na askari katika kilele cha Maadhimisho ya miaka 52 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania katika kikosi cha Usafirishaji wa anga (Air Wing) Ukonga jijini Dar es Salaam. 

 

 

 

 

 

RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA DKT. JOHN POMBE MAGUFULI, AMEMTHIBITISHA MKURUGENZI WA KITENGO CHA MAWASILIANO YA RAIS

unnamed

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, amemthibitisha Bw. Gerson Partinus Msigwa kuwa Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano ya Rais, (Director of Presidential Communication – DPC).

Taarifa iliyotolewa leo Jumatano Agosti 31,2016 na Katibu Mkuu Ikulu Bw. Peter Ilomo imeeleza kuwa Bw. Gerson Partinus Msigwa amethibitishwa kuanzia leo tarehe 31 Agosti, 2016 kushika wadhifa huo.

Kabla ya uthibitisho huo, Bw. Gerson Partinus Msigwa alikuwa Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano ya Rais, katika Ofisi ya Rais Ikulu kuanzia tarehe 17 Novemba, 2015.

Jaffar Haniu

Kaimu Mwandishi wa Habari wa Rais Msaidizi.

Dar es Salaam

31 Agosti, 2016