Daily Archives: October 14, 2016

RAIS DKT.JOHN POMBE MAGUFULI AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA NAIBU WAZIRI WA BIASHARA WA JAMHURI YA WATU WA CHINA IKULU JIJINI DAR ES SALAAM OKTOBA 14,2016

1

 

1.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Naibu Waziri wa Biashara kutoka Jamhuri ya Watu wa China Qian Keming aliyefika Ikulu pamoja na ujumbe wake kwa ajili ya mazungumzo Oktoba 14,2016

2 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Balozi wa China hapa nchini Dkt. Dkt. Lu youqing aliyefika Ikulu pamoja na ujumbe wa Naibu Waziri wa Biashara kutoka Jamhuri ya Watu wa China Qian Keming .

3Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Makamu wa Rais wa Benki ya EXIM ya China Sun Ping ambaye aliambatana na Naibu Waziri wa Biashara wa Jamhuri ya Watu wa China Qian Keming kwa ajili ya mazungumzo.

4Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Naibu Waziri wa Biashara kutoka Jamhuri ya Watu wa China Qian Keming watatu kutoka kulia aliyefika Ikulu pamoja na ujumbe wake kwa ajili ya mazungumzo. Wengine katika picha ni Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango wakwanza (kushoto) Makamu wa Rais wa Benki ya EXIM ya China Sun Ping wapili kutoka (kushoto) Balozi wa China hapa nchini Dkt. Dkt. Lu youqing watatu kutoka (kushoto),Pamoja na Waziri wa Viwanda Biashara na Uwekezaji Charles Mwijage wapili kutoka kulia.

5Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Naibu Waziri wa Biashara kutoka Jamhuri ya Watu wa China Qian Keming mara baada ya kumaliza mazungumzo yao Ikulu jijini Dar es Salaam.

6

 

7Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akijadiliana jambo na Balozi wa China hapa nchini Dkt. Lu youqing mara baada ya kumaliza mazungumzo ya pamoja na ujumbe wa Naibu Waziri wa Biashara kutoka Jamhuri ya Watu wa Jamhuri ya China uliofika Ikulu jijini Dar es Salaam