Daily Archives: August 25, 2017

RAIS MHE. DKT. JOHN POMBE MAGUFULI ASALIMIA WANANCHI WA FERRY KIGAMBONI WAKATI AKIELEKEA CHUO CHA KUMBUKUMBU YA MWALIMU NYERERE KWENYE UFUNGUZI WA KAMBI YA MAFUNZO YA VIJANA WA CCM ILIYOANDALIWA NA UMOJA WA VIJANA NA VYUO VIKUU.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akichukua Tiketi zake pamoja na chenchi mara baada ya kulipia huduma ya Kivuko wakati akielekea katika Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Kigamboni jijini Dar es Salaam.25 Agosti 2017.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana pamoja na kuzungumza na abiria mbalimbali wakati akisubiri kuvuka kwa kutumia usafiri wa Pantoni kuelekea katika Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Kigamboni jijini Dar es Salaam 25 Agosti 2017.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akimsikiliza Yusuph Ndemango ambaye ni mlemavu wakati alipomkuta ndani ya jengo la abiria lililopo upande wa Magogoni kabla ya kuvuka na Pantoni kuelekea katika Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Kigamboni jijini Dar es Salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiingia katika kivuko cha MV Kigamboni pamoja na abiria wengine wakati akivuka kuelekea upande wa pili wa Kigamboni jijini Dar es Salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiwa ndani ya Kivuko cha MV Kigamboni pamoja na abiria wengine wakati akivuka kuelekea upande wa pili wa Kigamboni jijini Dar es Salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiwasili ferry upande wa Kigamboni mara baada ya kushuka pamoja na abiria wengine kwenye pantoni la MV Kigamboni.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mama mmoja mara baada ya kuvuka upande wa Kigamboni jijini Dar es Salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akinunua chapati mara baada ya kuvuka upande wa Kigamboni wakati wa asubuhi 25 Agosti 2017.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiwasalimia wakazi wa Kigamboni mara baada ya kuvuka kwa kutumia usafiri wa Pantoni wakati katika Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Kigamboni jijini Dar es Salaam 25 Agosti 2017.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wa Shule ya Sekondari Minazini Kigamboni jijini Dar es Salaam 25 Agosti 2017.

Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiimba pamoja na wanachama wa CCM waliopo katika kambi ya mafunzo ya vijana iliyoandaliwa na Umoja wa vijana wa vyuo na Vyuo vikuu(CCM) katika Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam 25 agosti 2017.

 

Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wanachama wa CCM waliopo katika kambi ya mafunzo ya vijana iliyoandaliwa na Umoja wa vijana wa vyuo na Vyuo vikuu(CCM) katika ukumbi wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam 25 Agosti 2017.