Daily Archives: November 8, 2017

RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA MHE.DKT.JOHN POMBE MAGUFULI ATEMBELEA KIWANDA CHA SUKARI CHA KAGERA KILICHOPO WILAYANI MISENYI MKOANI KAGERA NA KUZUNGUMZA NA WANANCHI NA WAFANYAKAZI WA KIWANDA HICHO NOVEMBA 8,2017.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akikagua Mitambo ya kuchujia na kuvutia maji kwa ajili ya Mashamba ya Kiwanda cha Sukari cha Kagera Sugar, mitambo hiyo ipo pembezoni mwa Mto Kagera katika Wilaya ya Misenyi Novemba 8,2017.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mke wake Mama Janeth Magufuli  wakimsikiliza mtaalamu wa Kilimo aliyekuwa akielezea mambo mbalimbali katika mashamba ya miwa katika Kiwanda hicho cha Sukari cha Kagera Sugar kilichopo Misenyi mkoani Kagera.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwasikiliza wananchi wa Misenyi wakati wakitoa kero zao mbalimbali mara baada ya kuwasili katika kiwanda cha sukari cha Kagera akitokea kwenye mashamba ya miwa ya kiwanda cha Kagera Novemba 8,2017.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi wa Misenyi wakati wakitoa kero zao mbalimbali mara baada ya kuwasili wilayani Misenyi akitokea Bukoba mjini Novemba 8,2017.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mke wake Mama Janeth Magufuli pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum Kijuu wa pili kutoka kushoto , Waziri wa Kilimo Dkt. Charles Tizeba wa kwanza (kulia) wakisikiliza mtaalamu wa Kilimo aliyekuwa akielezea mambo mbalimbali katika mashamba ya miwa katika Kiwanda hicho cha Sukari cha Kagera Sugar kilichopo Misenyi mkoani Kagera.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na mkurugenzi wa Kiwanda cha Sukari cha Kagera  kilichopo Misenyi mkoani Kagera mara baada ya kuwasili katika kiwanda hicho Novemba 8,2017.

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akisikiliza mtaalamu wa Kilimo aliyekuwa akielezea namna mbegu za miwa zinavyoandaliwa katika mashamba ya miwa katika Kiwanda  cha Sukari cha Kagera Sugar kilichopo Misenyi mkoani Kagera.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Kilimo Dkt. Charles Tizeba, Charles Mwijage Waziri wa Viwanda,Biashara na Uwekezaji paoja na viongozi na wataalamu wa kilimo cha miwa katika mashamba ya miwa alipotembelea Kiwanda  cha Sukari cha Kagera Sugar kilichopo Misenyi mkoani Kagera Novemba 8,2017.

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia Shamba la miwa la Kiwanda hicho cha Sukari cha Kagera Sugar kilichopo Misenyi mkoani Kagera Novemba 8,2017.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na mkurugenzi wa  Shamba la miwa la Kiwanda cha Sukari cha Kagera  kilichopo Misenyi mkoani Kagera alipotembelea kiwanda hicho Novemba 8,2017.

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia namna uharibifu wa mazingira uliofanywa katika moja ya mito iliyopo kiwandani mara baada ya kukagua Shamba la miwa la Kiwanda cha Sukari cha Kagera Sugar kilichopo Misenyi mkoani Kagera Novemba 8,2017.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akifurahi kwa nyimbo nzuri ya mapokezi kutoka watoto wa chekechea mara baada ya kutembelea Shamba la miwa la Kiwanda cha Sukari cha Kagera kilichopo Misenyi mkoani Kagera Novemba 8,2017.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akikagua sukari kabla ya kufungwa kwenye mifuko yake alipotembelea kiwanda cha sukari cha Kagera kilichopo wilaya ya Misenyi mkoa wa Kagera Novemba 8, 2017.

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akishika moja ya mfuko wa sukari ambayo ipo tayari kwa kusafirishwa alipotembelea Kiwanda cha Sukari cha Kagera kilichopo Misenyi mkoani Kagera Novemba 8,2017.