Monthly Archives: March 2018

RAIS DKT.JOHN POMBE MAGUFULI AWAAPISHA MABALOZI WAWILI NA KUKUTANA NA WAGENI MBALIMBALI IKULU JIJINI DAR ES SALAAM.MACHI 21,2018

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika mazungumzo na Mauricio Ramos Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Millicom International Service LLC (wanne kutoka kushoto)ambayo inamiliki Kampuni ya simu ya Tigo aliyefika Ikulu pamoja na ujumbe wake.

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika mazungumzo na Watendaji Wakuu wa Kampuni ya FERROSTAAL kutoka nchini Ujerumani na Denmark Ikulu jijini Dar es Salaam. Wa kwanza kushoto ni Balozi wa Denmark Einar Hebogard Jensen aliyeongoza Ujumbe wa Kampuni hiyo Ikulu jijini Dar es Salaam.

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika mazungumzo na Watendaji Wakuu wa Kampuni ya FERROSTAAL kutoka nchini Ujerumani na Denmark Ikulu jijini Dar es Salaam.

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Meja Jenerali mstaafu Simon Marco Mumwi kuwa Balozi wa Tanzania nchini Urusi katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu jijini Dar es salaam Machi 21, 2018

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimkabidhi vitendea kazi baada ya kumuapisha Meja Jenerali mstaafu Simon Marco Mumwi kuwa Balozi wa Tanzania nchini Urusi katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu jijini Dar es salaam.Machi 21, 2018

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha IGP Mstaafu Ernest Jumbe Mangu kuwa Balozi wa Tanzania nchini Rwanda katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu jijini Dar es salaam.Machi 21, 2018

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akimkabidhi vitendea kazi baada ya kumuapisha IGP Mstaafu Ernest Jumbe Mangu kuwa Balozi wa Tanzania nchini Rwanda katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu jijini Dar es salaam.Machi 21, 2018

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwashuhudia Meja Jenerali mstaafu Simon Marco Mumwi na IGP Mstaafu Ernest Jumbe Mangu wakila kiapo cha maadili ya viongozi baada ya kuwaapisha kuwa Balozi wa Tanzania nchini Urusi na Rwanda katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu jijini Dar es salaam.Machi 21, 2018

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Suzan Kolimba, Katibu Mkuu Kiongozi balozi John Kijazi Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe Ramadhani Mwinyi katika picha ya pamoja na Meja Jenerali mstaafu Simon Marco Muwi na IGP Mstaafu Ernest Jumbe Mangu baada ya kuwaapisha kuwa Balozi wa Tanzania nchini Urusi na Rwanda katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu jijini Dar es salaam.Machi 21, 2018

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza Balozi mpya wa Tanzania nchini Rwanda IGP Mstaafu Ernest Mangu mara baada ya hafla fupi ya uapisho Ikulu jijini Dar es Salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Balozi mpya wa Tanzania nchini Urusi Meja Jenerali mstaafu Simon Marco Mumwi(kushoto) pamoja na Balozi mpya wa Tanzania nchini Rwanda IGP Mstaafu Ernest Mangu (kulia) mara baada ya hafla fupi ya uapisho Ikulu jijini Dar es Salaam.

RAIS DKT.JOHN POMBE MAGUFULI AENDESHA MKUTANO WA 11 WA BARAZA LA TAIFA LA BIASHARA IKULU JIJINI DAR ES SALAAM,MACHI 19,2018.

 

Sehemu ya wafanyabiashara wakiwa katika mkutano wa 11 wa Baraza la Taifa la Biashara unaoendeshwa na Mwenyekiti wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli Ikulu jijini Dar es salaam Machi 19, 2018.

Mwenyekiti wa Baraza la  Taifa la Biashara TNBC) Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akiwasili kuendesha mkutano wa 11 wa baraza hilo Kulia kwake ni   Waziri wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu Mhe. Jenista Joakim Mhagama na kushoto kwake ni  Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Prof. Elisante Ole Gabriel,Ikulu jijini Dar es salaam Machi 19, 2018.

Mwenyekiti wa Baraza la  Taifa la Biashara ITNBC) Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akisalimiana na Mwenyekiti wa Sekta Binafsi Dkt. Reginald Mengi  alipowasili kuendesha mkutano wa 11 wa baraza hilo Ikulu jijini Dar es salaam Machi 19, 2018. 

Mwenyekiti wa Baraza la  Taifa la Biashara TNBC) Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa meza kuu  na Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa  Waziri wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu Mhe. Jenista Joakim Mhagama na kushoto kwake ni  Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Prof. Elisante Ole Gabriel  na Mwenyekiti wa Sekta Binafsi Dkt. Reginald Mengi  akijiandaa kufungua  mkutano wa 11 wa baraza hilo Ikulu jijini Dar es salaam Machi 19, 2018.  

Sehemu ya wafanyabiashara wakiwa katika mkutano wa 11 wa Baraza la Taifa la Biashara unaoendeshwa na Mwenyekiti wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli Ikulu jijini Dar es salaam Machi 19, 2018.   

Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Prof. Elisante Ole Gabriel akizungumza katika mkutano mkuu wa 11 wa Baraza la Taifa la Biashara (TNDC),Ikulu jijini Dar es salaam Machi 19, 2018.

Sehemu ya wafanyabiashara wakiwa katika mkutano wa 11 wa Baraza la Taifa la Biashara unaoendeshwa na Mwenyekiti wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli Ikulu jijini Dar es salaam Machi 19, 2018.

Mwenyekiti wa  wa Sekta Binafsi Dkt. Reginald Mengi akizungumza katika mkutano mkuu wa 11 wa Baraza la Taifa la Biashara (TNDC),Ikulu jijini Dar es salaam Machi 19, 2018.

 

 

Mwenyekiti wa Baraza la  Taifa la Biashara TNBC) Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akiendesha  mkutano wa 11 wa baraza hilo Ikulu jijini Dar es salaam Machi 19, 2018.

 

Sehemu ya wafanyabiashara wakitoa changamoto zao wakati wa mkutano wa 11 wa Baraza la Taifa la Biashara unaoendeshwa na Mwenyekiti wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli Ikulu jijini Dar es salaam Machi 19,2018.