Daily Archives: July 13, 2018

MWENYEKITI WA CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) RAIS DKT.JOHN MAGUFULI AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA BARAZA JIPYA LA WADHAMINI WA CHAMA CHA MAPINDUZI CCM JIJINI DAR ES SALAAM.JULAI 13,2018

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Baraza jipya la wadhamini wa Chama cha Mapinduzi CCM Ikulu jijini Dar es Salaam.Kutoka kulia mstari wa kwanza ni Dkt. Haruni Kondo, Anna Abdallah(Mwenyekiti wa Baraza) na Jaji Mstaafu Mark Bomani wa kwanza kushoto. Wengine mstari wa nyuma kuanzia kulia ni Katibu Mkuu wa CCM Dkt. Bashiru Ally, Christopher Gachuma, John Chiligati, Balozi Mstaafu Daniel Ole Njoolay, Pandu Kificho pamoja na Hassan Mzee wa mwisho (kushoto) mstari wa nyuma.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na baadhi ya Wajumbe wa Baraza jipya la wadhamini wa Chama cha Mapinduzi CCM.Ikulu jijini Dar es Salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na mmoja wa wajumbe wa Baraza jipya la wadhamini wa Chama cha Mapinduzi CCM Hassan Mzee ambaye ni mmoja kati ya watu waliochanganya udongo wakati Tanganyika ilipoungana na Zanzibar na kuunda nchi moja ya Tanzania.Ikulu Jijini Dar es salaam.Julai 13,2018.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Dkt. John Pombe Magufuli akitoka kwenye kikao pamoja na Wajumbe wa Baraza jipya la wadhamini wa Chama cha Mapinduzi CCM Ikulu jijini Dar es Salaam.