Daily Archives: July 6, 2019

RAIS WA KENYA UHURU KENYATTA AMALIZA ZIARA YAKE BINAFSI YA SIKU MBILI CHATO MKOANI GEITA NAKUREJEA NCHINI KWAKE

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na mgeni wake Rais wa Kenya Mheshimiwa Uhuru Kenyatta katika uwanja wa ndege wa Chato mara baada ya kumaliza ziara yake binafsi ya siku mbili Chato mkoani Geita.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimsindikiza mgeni wake Rais wa Kenya Mheshimiwa Uhuru Kenyatta wakati wakipita kwenye Gadi ya Heshma iliyoandaliwa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania JWTZ katika uwanja wa Ndege wa Chato mkoani Geita.

 

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mgeni wake Rais wa Kenya Mheshimiwa Uhuru Kenyatta wakati wakisikiliza nyimbo iliyokuwa ikiimbwa na wanakwaya wa Mwagazege ya Chato kabla ya Rais Kenyatta kuondoka na kurejea nchini Kenya.

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wanahabari mara baada ya mazungumzo yake na mgeni wake Rais wa Kenya Mheshimiwa Uhuru Kenyatta Chato mkoani Geita.

 

Rais wa Kenya Mheshimiwa Uhuru Kenyatta akimsalimia Mama mzazi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli, Bibi Suzana Magufuli ambaye anapatiwa matibabu kijijini kwake Mlimani Chato mkoani Geita kabla ya kuondoka kurejea Kenya mara baada ya kumaliza ziara yake binafsi ya siku mbili.

Rais wa Kenya Mheshimiwa Uhuru Kenyatta akizungumza na wanahabari mara baada ya mazungumzo yake na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli.

Rais wa Kenya Mheshimiwa Uhuru Kenyatta akiweka shada la maua katika moja ya makaburi ya Familia ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli yaliyopo katika kijiji cha Mlimani Chato wakati akiwa katika ziara yake binafsi ya siku mbili.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha na mgeni wake Rais wa Kenya Mheshimiwa Uhuru Kenyatta kabla ya kuanza mazungumzo yao Chato mkoani Geita.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na mgeni wake Rais wa Kenya Mheshimiwa Uhuru Kenyatta mara baada ya mazungumzo yao Chato mkoani Geita.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na mgeni wake Rais wa Kenya Mheshimiwa Uhuru Kenyatta ambaye aliambatana na ujumbe wake kutoka Kenya katika ziara yake binafsi ya siku mbili katika kijiji cha Mlimani Chato Mkoani Geita.

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na mgeni wake Rais wa Kenya Mheshimiwa Uhuru Kenyatta kabla ya kuondoka katika kijiji cha Mlimani Chato na kurejea nchini kwake Kenya.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na mgeni wake Rais wa Kenya Mheshimiwa Uhuru Kenyatta kabla ya kuondoka katika kijiji cha Mlimani Chato na kurejea nchini kwake Kenya.