Daily Archives: October 8, 2019

RAIS MHE. DKT. MAGUFULI AFUNGUA BARABARA YA SUMBAWANGA –KANAZI KM 75 PIA AFUNGUA MIRADI YA MAENDELEO NKASI MKOANI RUKWA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akivuta utepe pamoja na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isaack Kamwelwe kuashiria ufunguzi wa barabara ya Sumbawanga-Kanazi km 75 iliyokamilika kujengwa kwa kiwango cha lami katika sherehe zilizofanyika Kanazi mkoani Rukwa. 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi wa Kanazi mara baada ya kufungua barabara ya Sumbawanga-Kanazi km 75 iliyokamilika kujengwa kwa kiwango cha lami katika sherehe zilizofanyika Kanazi mkoani Rukwa. 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
akisoma mango kabla ya kuikata utepe kuzindua barabara ya
Sumbawanga-Kanazi mkoani Rukwa. Oktoba 8, 2019

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mkewe Mama Janeth Magufuli watano kutoka kulia walioshika utepe, Wabunge wa mkoa wa Rukwa, Kamati ya Miundombinu, Mawaziri, akakata utepe kufungua barabara ya Sumbawanga-Kanazi km 75 iliyokamilika kujengwa kwa kiwango cha lami katika sherehe zilizofanyika Kanazi mkoani Rukwa. 

Sehemu ya Barabara ya Sumbawanga-Kanazi km 75 iliyokamilika kujengwa kwa kiwango cha lami kama inavyoonekana.

Sehemu ya barabara ya Sumbawanga-Kanazi  yenye urefu wa kilometa
75 iliyozinduliwa  na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.
John Pombe Magufuli Oktoba 8,2019

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akikagua moja ya chumba cha hospitali ya Wilaya ya Nkasi mara baada ya kuweka jiwe la msingi.

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akikagua gril la dirisha la moja ya chumba cha hospitali ya Wilaya ya Nkasi mara baada ya kuweka jiwe la msingi.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akifungua kituo cha Afya cha Nkomolo Nkasi mkoani Rukwa.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mkewe Mama Janeth Magufuli, Waziri wa Afya Ummy Mwalimu, Waziri wa Tamisemi Selemani Jafo, Waziri wa Mambo ya Ndani Kangi Lugora, Mbunge wa Nkasi Ally Keissy, akikata utepe kuashiria ufunguzi kituo cha Afya cha Nkomolo Nkasi mkoani Rukwa.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza Mbunge wa Nkasi Ally Keissy mara baada ya kuweka jiwe la msingi ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Nkasi mkoani Rukwa.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mkewe Mama Janeth Magufuli, wakiangalia zoezi la uandikishaji la wapiga kura wa Viongozi wa Serikali za mitaa Nkasi mkoani Rukwa.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
akishuhudia wananchi wakijiandikisha katika daftari la mpinga kura
eneo la Nkomolo Wilaya ya Nkasi mkoani Rukwa leo Oktoba 8, 2019.
Akitoa maelezo kushoto ni Katibu Tawala Msaidizi wilaya ya Nkasi Bw.
Albinus Mugonya.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na mwanachi wa Nkasi Albina Kasanya (74) ambaye alikuwa amemaliza kujiandikisha katika kituo cha Hospitali ya Wilaya ya Nkasi mkoani Rukwa.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Wanafunzi wa Shule za Msingi na Sekondari wa Nkasi waliokuwa pembezoni mwa majengo ya hospitali ya Wilaya ya Nkasi mkoani Rukwa. 

Sehemu ya Majengo ya Hospitali ya Wilaya ya Nkasi ambayo ipo katika hatua za mwisho kukamilika Nkasi mkoani Rukwa.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimsikiliza Bi Paskalia Mikael mara baada ya kusimama katika kijiji cha Chala mkoani Rukwa wakati akielekea Nkasi.

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wanachi wa Chala mara baada ya kuwasili kijijini hapo.

Wanafunzi wa Kasu Sekondary Wakishangilia mara baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kuwasili katika kijiji hicho.

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wanachi wa Kasu mkoani Rukwa

Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akituza viaja wa kwaya ya JKT
walipotumbuiza wakati wa mkutano wa hadhara Mjini  Nyamanyere wilaya ya Nkasi Mkoa wa Rukwa.  Oktoba 8, 2019

 

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwahutubia wananchi wa Namanyere Nkasi mkoani Rukwa mara baada ya kuwasili akitokea Sumbawanga.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea na Mama Felista Mkombo baada ya kuamuru ofisi za Mkjuu wa Wilaya na Mkuu wa Polisi Wilayani Nkasi kumpa  shillingi milioni 15 kama fidia ya kuibiwa ng’ombe zake 25 Mjini Namanyere wilayani Nkasi

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akitoa maelekezo kwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Kangi Lugora mara baada ya kuhutubia wanachi wa Namanyere Nkasi mkoani Rukwa.