Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiondoka na Gari yake Binafsi katika Makao Makuu ya Ofisi za CCM White House Dodoma kuelekea Ofisi za CCM Mkoa Makole Dodoma na badae kurejea katika Ikulu ya Chamwino leo mara baada ya kuchukua fomu ya kuomba ridhaa ya Chama kuteuliwa kuwa Mgombe katika Kiti cha Urais katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika baadae mwaka huu.
Daily Archives: June 17, 2020
MWENYEKITI WA CCM RAIS MHE. DKT. MAGUFULI AKABIDHI FOMU YA KUTAFUATA WADHAMINI OFISI CCM MKOA DODOMA MARA BAADA YA KUCHUKUA FOMU YA KUGOMBEA URAIS MAPEMA LEO .
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Rais Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akikabidhi Fomu ya kutafuta wa dhamini wa chama baada kuchukua fomu ya kuomba kuteuliwa kugombea Urais kwa Tiketi ya CCM katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika baadae mwaka huu Dodoma leo tarehe 17 JUNI 2020.
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Rais Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akipeana mkono na katibu wa chama cha mapinduzi mkoa wa Dodoma Bi. Jamila Yusufu. baada ya kumkabidhi Fomu ya kutafuta wa dhamini ndani ya chama, ilikutimiza vigezo vya kuomba kuteuliwa kugombea Urais kwa Tiketi ya CCM katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika baadae mwaka huu Dodoma leo tarehe 17 JUNI 2020.
Katibu wa chama cha mapinduzi mkoa wa Dodoma Bi. Jamila Yusufu akimpongeza Mhe. Rais Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli baada ya kumkabidhi Fomu ya kutafuta wa dhamini ndani ya chama, ilikutimiza vigezo vya kuomba kuteuliwa kugombea Urais kwa Tiketi ya CCM katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika baadae mwaka huu Dodoma leo tarehe 17 JUNI 2020