Daily Archives: July 11, 2020

WENYEKITI WA CHAMA CHA MAPINDUZI CCM RAIS MHE. DKT. MAGUFULI ACHAGULIWA NA MKUTANO MKUU WA CCM KUWA MGOMBEA URAIS KWA TIKETI YA CCM KATIKA UCHAGUZI MKUU UTAKAOFANYIKA BADAE MWAKA HUU

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Rais wa Jamhuri ya Muungano Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM, wageni mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi mara baada ya kuteuliwa kuwa Mgombea Urais kwa Tiketi ya CCM katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika hapo badae mwaka huu.

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Rais wa Jamhuri ya Muungano Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa ameketi pamoja na Waziri Mkuu Mstaafu Cleopa David Msuya wakati akisubiri kutangazwa kwa matokeo mara baada ya Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM kumpigia kura.

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Rais wa Jamhuri ya Muungano Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Rais Mstaafu wa Awamu ya tatu Benjamin Mkapa wakati akisubiri matokeo mara baada ya Wajumbe wa Mkutano Mkuu kupiga kura.

 Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akipiga makofi pamoja na Wajumbe wengine walioshiriki Mkutano Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM uliofanyika katika Ukumbi wa Jakaya Kikwete jijini Dodoma.

 Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan akiwa anapiga makofi katika mkutano huo Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM ambao ulimchagua Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Rais wa Jamhuri ya Muungano Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kuwa Mgombea Urais katika Uchaguzi utakaofanyika baadae mwaka huu. Rais Dkt. Magufuli alimchagua tena Makamu wa Rais kuwa Mgombea Mwenza.

Wajumbe Mbalimbali wa Mkutano Mkuu wa CCM wakishangilia wakati Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Rais wa Jamhuri ya Muungano Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli alipokuwa akihutubia katika mkutano uliofanyika katika Ukumbi wa Jakaya Kikwete Conventional Center jijini Dodoma.

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Rais wa Jamhuri ya Muungano Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwahutubia wajumbe wa mkutano mkuu wa Taifa wa CCM  mara baada ya kupitishwa  na Mkutano Mkuu kwa kura zote sawa na Asilimia mia.

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Rais wa Jamhuri ya Muungano Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akipunga mkono wakati akiondoka katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Conventional Center mara baada ya Mkutano Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM uliompigia kura zote kwa ajili ya kugombea Urais katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika baadae mwaka huu.