Monthly Archives: November 2020

RAIS MHE. DKT. MAGUFULI AMUAPISHA MHE. KASSIM MAJALIWA MAJALIWA (MB) KUWA WAZIRI MKUU WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA MKOANI DODOMA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb) kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika hafla fupi iliyofanyika katika viwanja vya Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma leo tarehe 16 Novemba, 2020.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Profesa Palamagamba Kabudi (Mb) kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki katika hafla fupi iliyofanyika katika viwanja vya Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma leo tarehe 16 Novemba, 2020.

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) kuwa Waziri wa Fedha na Mipango katika hafla fupi iliyofanyika katika viwanja vya Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma leo tarehe 16 Novemba, 2020

RAIS MAGUFULI AHUTUBIA NA KULIFUNGUA BUNGE LA 12 DODOMA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia pamoja na kulifungua rasmi Bunge hilo la 12 leo tarehe 13 Novemba 2020 jijini Dodoma

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Rais wa Zanzibar Dkt. Hussein Ali Mwinyi, Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Mzee Ali Hassan Mwinyi pamoja na Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt. Jakaya Kikwete na Spika  wa Bunge Mhe.Job Ndugai mara baada ya kufungua Bunge la 12 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania jijini Dodoma leo

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli wakiwa katika Picha ya pamoja na Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete na  Rais Mstaafu wa Awamu ya pili Mzee Ali Hassan Mwinyi Dodoma  Mara baada ya kumaliza kulihutubia Bunge.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Mhe. Ali Hassan Mwinyi  mara baada ya kufungua Bunge la 12 leo tarehe 13 Novemba 2020 jijini Dodoma. Kulia ni Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete .

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika Picha ya Pamoja na viongozI wa serikali wabunge ,Spika Mhe. Job Ndugai , Rais Mstaafu wa Awamu ya pili Mzee Ali Hassan Mwinyi na Rais mstaafu awamu ya Nne Dkt .Jakaya Mrisho Kikwete. Nje ya ukumbi wa Bunge Mara baada ya kumaliza hotuba yake ya kulifungua Bunge la 12 la jamhuri ya muungano wa Tanzania.