Rais Dkt.Jakaya Mrisho kikwete akimtambulisha kwa Rais Museveni Mkuu wa Majeshi ya Tanzania Jenerali Davies Mwamunyange muda mfupi baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere kwa ziara ya kikazi ya siku moja September 10,2014 Kushoto ni Inspekta Jenerali wa Polisi Ernest Mangu.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete na mgeni wake Rais Yoweri Kaguta Museveni wa Uganda wakikagua gwaride la Heshima lililoandaliwa na jeshi la Wananchi wa Tanzania September 10,2014.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete na Rais Yoweri Museveni wa Uganda wakikagua ngoima za utamaduni September 10,2014
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimkaribisha ikulu jijini Dar es Salaam Rais Yoweri Kaguta Museveni wa Uganda na kufanya naye mazungumzo September 10,2014.Rais Museveni yupo nchini Tanzania kwa ziara ya kikazi ya siku moja
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza Ikulu jijini Dar es Salaam September 11,2014 na Jaji Sophia Akkufo Rais wa Mahakama ya Haki za Binadamu ya Afrika(AFHPR) aliyemaliza muda wake ,
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiagana na balozi wa Ufaransa aliyemaliza muda wake nchini Mhe.Marcel Escure wakati balozi huyo alipokwenda kumuaga Ikulu jijini Dar es Salaam September 11,2014
MAMA SALMA KIKWETE AZINDUA MTAMBO WA 10,000 WA BIOGAS KITAIFA BAGAMOYO SEPTEMBER 10, 2014.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akitembelea maonesho ya biogas yaliyofanyika katika Kijiji cha Kondo tarehe 10.9.2014. Mkurugenzi Mkuu wa CARMATEC Ndugu Elifariji Makongoro (kulia) akimpatia maelezo mbalimbali ya kazi zinazofanywa na shirika hilo. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mheshimiwa Mwantumu Mahiza.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akitembelea maonesho ya biogas yaliyofanyika katika Kijiji cha Kondo tarehe 10.9.2014. Mkurugenzi Mkuu wa CARMATEC Ndugu Elifariji Makongoro (kulia) akimpatia maelezo mbalimbali ya kazi zinazofanywa na shirika hilo. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mheshimiwa Mwantumu Mahiza.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akikata utepe huku akishirikiana na viongozi mbalimbali ikiwa ni ishara ya uzinduzi rasmi wa mtambo wa wa 10,000 wa Biogas hapa nchini. Mtambo huo unaomilikiwa na Ndugu Bakari Seif na Mkewe Mwanaidi Said (wa pili na wa tatu kutoka kushoto). Wa kwanza kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Ndugu Eliakim Maswi, kulia kwa Mama Salma ni Mkuu wa Mkoa wa Pwani Ndugu Mwantumu Mahizana. Aliyesimama kushoto ni Mwenyekiti wa Kijiji cha Kondo Ndugu Ramadhan Seleman akifuatiwa na Mkurugenzi Mkuu wa CARMATEC Ndugu Elifariji Makomgoro.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akipata maelezo kutoka kwa Ndugu Andrew Mvungi, Mtaalam wa usanifu na ujenzi wa mitambo ya biogas kutoka Tanzania Domestic Biogas Pragram ya huko Arusha kuhusiana na matumizi mbalimbali ya biogas kama vile kupikia na nishati ya umeme.