Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Bw. Leonidas Gama (kushoto) akimkaribisha Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Y. Sefue (kulia) ofisini kwake mara baada ya Katibu Mkuu Kiongozi kuwasili ofisini hapo tayari kuanza ziara yake ya kikazi Mkoani humo, Septemba 19, 2014.
Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Y. Sefue (kushoto), akisaini kitabu cha wageni ofisini kwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Bw. Leonidas Gama (wa pili kushoto). Kulia ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Kilimanjaro Dk. Issa Feisal.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Bw. Leonidas Gama akizungumza machache kabla ya kumkaribisha Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Y. Sefue, kuendesha mkutano Wadau wa Uwekezaji Mkoani Kilimanjaro, uliofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Septemba 19, 2014.
Baadhi ya Watendaji kutoka Ofisi ya Rais Ikulu na Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI wakifuatilia kwa makini mkutano Wadau wa Uwekezaji Mkoani Kilimanjaro uliofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Septemba 19, 2014.
Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Uchumi ya Kilimanjaro, Bibi D. Kileo akiwasilisha moja ya mada katika mkutano Wadau wa Uwekezaji Mkoani Kilimanjaro, uliofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Septemba 19, 2014.
Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Y. Sefue (kulia), akiendesha Mkutano wa Wadau wa Uwekezaji Mkoani Kilimanjaro. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Bw. Leonidas Gama. Mkutano huo ulifanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Septemba 19, 2014.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Bw. Eliakim Maswi, akichangia hoja katika mkutano wa Wadau wa Uwekezaji Mkoani Kilimanjaro, uliofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Septemba 19, 2014.
Msanifu Majengo wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi, Bw. Faustin Mosha (aliyenyoosha mkono) akitoa maelezo kuhusu uendelezaji wa eneo la Lokolova lililopo wilaya ya Moshi Vijijini wakati Katibu Mkuu Kiongozi na ujumbe wake walipotembelea eneo hilo. Wa pili kushoto ni Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI Bw. Jumanne A. Sagini.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Kilimanjaro Dk. Issa Feisal (aliyesimama), akimkaribisha Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Y. Sefue kuzungumza na Watumishi wa Halmashauri ya Mji wa Moshi na Wilaya zake katika kikao kilichofanyika katika ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Septemba 19, 2014.
Baadhi ya Watumishi wa Halmashauri ya Mji wa Moshi na Wilaya zake wakimsikiliza Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Y. Sefue, katika kikao kilichofanyika katika ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Septemba 19, 2014.
Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Y. Sefue, akizungumza na Watumishi wa Halmashauri ya Mji wa Moshi na Wilaya zake katika kikao kilichofanyika katika ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Septemba 19, 2014.
Afisa Rasilimaliwatu wa Wakala wa Barabara Mkoani Kilimanjaro, Bw. Richard Mushi, akiuliza swali katika kikao cha Katibu Mkuu Kiongozi na Watumishi wa Halmashauri ya Mji wa Moshi na Wilaya zake na Taasisi za Serikali Mkoani humo, kikao kilichofanyika katika ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Septemba 19, 2014.
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, Bw. Jumanne A. Sagini akitoa ufafanuzi wa hoja zilizotolewa na Watumishi katika kikao kilichofanyika katika ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Septemba 19, 2014.
Mkuu wa Chuo cha Kikuu cha ushirika na biashara cha Moshi (MUCCOBS) Profesa Joseph Bee, akitoa neno la shukrani kwa Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Y. Sefue pamoja na ujumbe wake kwa kufanya ziara ya kikazi waliyoifanya Mkoani Kilimanjaro, Septemba 19, 2014.