RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA MHE.DKT.JOHN POMBE MAGUFULI AFUNGUA VIWANDA KAHAMA NA SINGIDA.MACHI 11,2018.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akivuta utepe pamoja na viongozi wengine kuashiria ufunguzi wa kiwanda kikubwa cha Kusindika na kuzalisha mafuta ya Alizeti cha Mount Meru Millers kilichopo mkoani Singida. Kiwanda hicho kina uwezo wa kuzalisha tani elfu tisini za mafuta ya alizeti kwa mwaka.Machi 11,2018.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akikata utepe kuashiria ufunguzi wa kiwanda hicho kikubwa cha kusindika Alizeti cha Mount meru millers kilichopo mkoani Singida. Wengine katika picha ni Mkuu wa mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi, Waziri wa Mambo ya Ndani Dkt. Mwigulu Nchemba, mmiliki wa Kiwanda hicho Atul Mittal mwenye nguo nyeupe na Waziri wa Viwanda na Biashara Charles Mwijage.

 

 

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi waliohudhuria hafla ya uzinduzi wa Kiwanda cha kusindika Alizeti cha Mount Meru Millers kilichopo mkoani Singida.Machi11,2018.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwpungia mkono wananchi  alipokuwa akielekea kukagua shughuli mbalimbali za kiwanda hicho cha usindikaji wa Alizeti kilichopo mkoani Singida.

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akielekea kwenda kukagua shughuli mbalimbali za kiwanda hicho cha usindikaji wa Alizeti kilichopo mkoani Singida.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiombewa na viongozi wa Kidini kutoka Singida mara baada ya kufungua kiwanda hicho cha usindikaji wa Alizeti.Machi 11,2018.

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwasalimia wananchi waliohudhuria hafla ya uzinduzi wa kiwanda hicho cha usindikaji wa Alizeti.

Mkuu wa mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi akifurahia jambo na Waziri wa Mambo ya Ndani Dkt. Mwigulu Nchemba wakati wa hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kabla ya uzinduzi wa kiwanda hicho kikubwa cha Usindikaji wa Alizeti mkoani Singida.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza mmiliki wa Kiwanda cha Mount Meru Millers Atul Mittal mara baada ya kumaliza kutoa hotuba yake ya uzinduzi wa kiwanda hicho cha usindikaji wa Alizeti mkoani Singida.Machi 11,2018.

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi wa Kagongwa Kahama mkoani Shinyanga wakati akielekea mkoani Singida.Machi 11,2018.

Wananchi wa Kagongwa Kahama mkoani Shinyanga wakishangilia wakati Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli alipokuwa akiwasili katika eneo hilo wakati akielekea mkoani Singida.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akifungua kiwanda cha Kahama Oil mills kilichopo Kahama mkoani Shinyanga.Machi 11,2018.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akikata utepe kuashiria ufunguzi wa kiwanda cha Kahama Oil mills kilichopo Kahama mkoani Shinyanga.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa amekalia moja ya kiti kilichotengenezwa na kiwanda cha Kahama Oil mills wakati akikagua bidhaa zinazo tengenezwa kiwandani hapo Kahama mkoani Shinyanga. Pembeni yake ni Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Bi. Zainab Telak.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia moja ya mabomba ya plastik yanayo tengenezwa katika kiwanda hicho cha Kahama Oil mills kilichopo Kahama mkoani Shinyanga.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wafanyakazi wa Kiwanda cha Kahama Oil mills mara baada ya kukifungua.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi wa Tinde mkoani Shinyanga wakati akielekea mkoani Singida.

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi wa Igunga mkoani Tabora wakati akielekea mkoani Singida.Machi 11,2018.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *