RAIS DKT. MAGUFULI AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA BALOZI WA MOROCCO HAPA NCHINI ALIYEAMBATANA NA UJUMBE KUTOKA NCHINI KWAO IKULU JIJINI DAR ES SALAAM

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Kiongozi wa Ujumbe kutoka nchini Morocco Balozi Mohamed Methqal ambaye ni Mkurugenzi mkuu wa Wakala wa Ushirikiano wa Kimataifa wa Morocco mara baada ya kuwasili Ikulu jijini Dar es Salaam. katikati ni Balozi wa Morocco hapa nchini Abdelilah Benryane akishuhudia.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo kuhusu ujenzi wa Uwanja wa Mpira wa Miguu utakaokuwa na uwezo wa kuingiza watazamaji zaidi ya 85,000 mkoani Dodoma huku Balozi wa Morocco hapa nchini Abdelilah Benryane wanne kutoka (kushoto) pamoja na Kiongozi wa Ujumbe kutoka nchini Morocco Balozi Mohamed Methqal watatu kutoka kushoto pamoja na ujumbe huo wakisikiliza.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika kikao na Balozi wa Morocco hapa nchini Abdelilah Benryane ambaye aliambatana pamoja na Kiongozi wa Ujumbe kutoka nchini Morocco Balozi Mohamed Methqal ambaye ni Mkurugenzi mkuu wa Wakala wa Ushirikiano wa Kimataifa wa Morocco, Ikulu jijini Dar es Salaam. Wengine katika picha ni Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki Profesa Palamagamba Kabudi, Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara nchini Patrick Mfugale pamoja na wajumbe wengine.

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo kuhusu ujenzi wa Uwanja wa Mpira wa Miguu utakaokuwa na uwezo wa kuingiza watazamaji zaidi ya 85,000 mkoani Dodoma huku Balozi wa Morocco hapa nchini Abdelilah Benryane wanne kutoka (kushoto) pamoja na Kiongozi wa Ujumbe kutoka nchini Morocco Balozi Mohamed Methqal watatu kutoka kushoto pamoja na ujumbe huo wakisikiliza.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Morocco hapa nchini Abdelilah Benryane wasabi kutoka kushoto akifatiwa na Kiongozi wa Ujumbe kutoka nchini Morocco Balozi Mohamed Methqal ambaye ni Mkurugenzi mkuu wa Wakala wa Ushirikiano wa Kimataifa wa Morocco pamoja na Ujumbe wao. Wengine katika picha ni ni Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki Profesa Palamagamba Kabudi wasabi kutoka kulia, Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara nchini TANROADS Mhandisi Patrick Mfugale wasita kutoka kulia, Balozi Zuhuru Bundala wakwanza kulia pamoja na wajumbe wengine Ikulu jijini Dar es Salaam.

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia mfano wa Uwanja mkubwa wa mpira wa miguu utakaojengwa Jijini Dodoma kwa ufadhili wa Mfalme wa Morocco Mohamed VI. Uwanja huo utakuwa na uwezo wa kuchukua watazamaji 85,000 (normal capacity) waliokaa kwenye viti lakini pia utaweza kubeba washabiki hadi105,000 kama walivyopanga. Kwa nje uwanja huo utakuwa na muonekano kama mlima Kilimanjaro hivyo kuzidi kupamba madhari ya mjii mkuu wa Tanzania mkoani Dodoma. 

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *