RAIS MHE. DKT. MAGUFULI AKUTANA NA UJUMBE KUTOKA WIZARA YA ULINZI YA UJERUMANI, WIZARA YA NJE YA UJERUMANI PAMOJA NA BALOZI WA UJERUMANI HAPA NCHINI IKULU JIJINI DAR ES SALAAM

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Balozi wa Ujerumani hapa nchini Dkt. Detlef Waechter mara baada ya kuwasili Ikulu jijini Dar es Salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Malte Loknitz kutoka Ujerumani (kushoto) ambaye alikuwa akitambulishwa na Balozi wa Ujerumani hapa nchini Dkt. Detlef Waechter katikati mara baada ya kuwasili Ikulu jijini Dar es Salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akijadiliana jambo na Balozi wa Ujerumani hapa nchini Dkt. Detlef Waechter mara baada ya kumaliza kikao chao na ujumbe kutoka nchini Ujerumani Ikulu jijini Dar es Salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Balozi wa Ujerumani hapa nchini Dkt. Detlef Waechter mara baada ya mazungumzo yao pamoja na Ujumbe kutoka nchini Ujerumani Ikulu jijini Dar es Salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Ujerumani hapa nchini Dkt. Detlef Waechter wasita kutoka kushoto, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dkt. Hussein Mwinyi watatu kutoka kushoto, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Wananchi wa Tanzania Jenerali Venance Mabeyo watatu kutoka kulia pamoja na wajumbe wengine kutoka Ujerumani na Tanzania.

Mjumbe kutoka nchini Ujerumani Malte Loknitz akizungumza na vyombo vya habari kwa lugha ya Kiswahili mara baada ya kikao chao na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli Ikulu jijini Dar es Salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza Mjumbe kutoka nchini Ujerumani Malte Loknitz mara baada ya kuzungumza na vyombo vya habari Ikulu jijini Dar es Salaam. 

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *