RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA MHESHIMIWA JAKAYA MRISHO KIKWETE AMEWASILI NCHINI NAMIBIA MACHI 20, 2015 KWA ZIARA YA SIKU TATU

1dfvfvf

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amewasili nchini Namibia jioni ya leo, Ijumaa, Machi 20, 2015 kwa ziara ya siku tatu katika nchini hiyo ambako atahudhuria sherehe mbili kubwa na muhimu kwa taifa la Namibia.

Rais Kikwete na ujumbe wake amewasili kwenye Uwanja wa Kimataifa wa Ndege wa Hosea Kutako mjini Windhoek kiasi cha saa 12 jioni kwa saa za Namibia tayari kwa ziara  hiyo.

Wakati wa ziara hiyo, Rais Kikwete atahudhuria Sherehe za Miaka 25 ya Uhuru wa Namibia na pia kuhudhuria Sherehe za Kuapishwa Rais wa Tatu wa Jamhuri ya Namibia, Mheshimiwa Hage Gotrified  Geinagob.

 

 

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *