



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, tarehe 06 Septemba, 2021 amewasili katika wilaya ya Serengeti mkoani Mara akiwa na kundi la wapiga picha wa kipindi cha Royal Tour kwa ajili ya kuendelea kuonesha na kuelezea vivutio vya utalii vilivyopo nchini kupitia filamu itakayoandaliwa na timu hiyo.
Mhe. Rais Samia amewaambiwa wananchi wa Wilaya hiyo waliojitokeza kumpokea kuwa filamu hiyo itakapokamilika itatangaza maeneo yote yenye vivutio vya utalii nchini na kuchochea uchumi wa nchi kupitia watalii, wawekezaji na wafanyabiashara.
Aidha, Mhe. Rais amesema filamu hiyo pia itaelezea hali halisi ya siasa zilivyo nchini tofauti na baadhi ya mataifa mengine inavyoelezea.
Amesema kwa sasa wahisani wengi wametoka katika utoaji wa misaada na kujikita katika biashara, hivyo filamu hiyo itasaidia kueleza na kuonesha maeneo mbalimbali ya utalii ambayo yatatoa furza za biashara na uwekezaji.
Pia, Mhe. Rais Samia amewahakikishia wananchi wa Wilaya ya Serengeti kuwa ahadi zote zilizotolewa na Chama cha Mapinduzi (CCM) wakati wa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020 zitatekelezwa.