Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza kwa njia ya Simu na Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Mhe. Antony Blinken, leo tarehe 06 Julai, 2021 Ikulu Jijini Dodoma ambapo kwenye mazungumzo yao Waziri huyo amemhakikishia Mhe. Rais Samia kuwa Serikali ya Marekani itaendelea kukuza ushirikiano na Serikali ya Tanzania katika Nyanja mbalimbali za maendeleo.