Daily Archives: January 24, 2023

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.  Samia Suluhu Hassan amefanya utenguzi wa nafasi za Viongozi wafuatao:-

  1. Bw. Reuben Ndiza Mfune, Mkuu wa Wilaya ya Mbarali;
  • Bw. Msongela Nitu Palela, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma, Mara;
  • Bw. Michael Augustino Matomora, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Singida;
  • Bw. Linno Pius Mwageni, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu, Shinyanga; na
  • Bw. Sunday Deogratius Ndori, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa, Njombe.

Utenguzi huu ulianza tarehe 22 Januari, 2023.