Category Archives: Uzinduzi/Ufunguzi

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ametengua uteuzi wa Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni Mkoani Dar es Salaam Bw. Aron Titus Kagurumjuli.

Mhe. Rais Magufuli ametengua uteuzi huo kuanzia leo tarehe 16 Februari, 2021.

Uteuzi wa Mkurugenzi mwingine wa Manispaa hiyo utafanywa baadaye.