Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amefanya mabadiliko ya vituo kwa Mabalozi wawili (02) na uteuzi wa Balozi mmoja (01) kama ifuatavyo:
- Amempangia Balozi Humphrey Herson Polepole kuiwakilisha Tanzania nchini Cuba. Kabla ya uteuzi huu Balozi Polepole alikuwa Balozi wa Tanzania, nchini Malawi.
- Amemteua Balozi Lt. Jenerali (mstaafu) Yacoub Mohamed kuiwakilisha Tanzania katika Falme za Kiarabu (UAE). Kabla ya uteuzi huu, Balozi Mohamed alikuwa Balozi wa Tanzania nchini Uturuki.
Uteuzi na kupangiwa Kituo
- Amemteua Bw. Iddi Seif Bakari kuwa Balozi na kumpangia Ubalozi nchini Uturuki. Kabla ya uteuzi huu, Bw. Bakari alikuwa Konseli Mkuu, Dubai.
Tarehe ya uapisho wa Balozi Bakari itatangazwa baadae.