Monthly Archives: October 2023

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

RAIS SAMIA APOKEA RIPOTI YA UTAFITI WA AFYA YA UZAZI NA MTOTO

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan ameiagiza Wizara ya Afya na Ofisi ya Rais – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kuhakikisha hospitali zote nchini zinakuwa na wodi maalum za watoto wachanga.

Aidha, Rais Samia amewataka kuhakikisha wodi hizo zinakuwa na watumishi wenye ujuzi, vifaa tiba na dawa muhimu kwa watoto hao wachanga.

Rais Samia ametoa agizo hilo leo wakati wa uzinduzi wa matokeo ya utafiti wa afya ya uzazi na mtoto na viashiria vya malaria (2022) na ugawaji wa magari ya kubebea wagonjwa na vifaa tiba katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere.

Rais Samia pia amezitaka Wizara ya Afya, TAMISEMI na Wizara ya Maendeleo ya Jamii kushirikiana kubeba ajenda ya kupambana na udumavu wa watoto chini ya miaka 5 na kuiwekea mpango wa utekelezaji. 

Vile vile Rais Samia amezitaka Wizara hizo kupanua wigo wa uelimishaji na uhamasishaji wa masuala ya lishe ili kupunguza zaidi kiwango cha udumavu nchini ambacho kimepungua kutoka 34% mwaka 2015/16 hadi 30% mwaka 2022. 

Kwa upande mwingine, Rais Samia amesema matokeo chanya yaliyobainishwa na utafiti huu yanadhihirisha matokeo ya uwekezaji mkubwa unaoendelea kufanywa na serikali kwenye sekta ya afya.

Rais Samia amegawa seti 123 za vifaa vya huduma kwa watoto wachanga na wenye uzito pungufu, mashine 125 za mionzi, mashine 140 za kutibu dalili za awali za saratani ya mlango wa kizazi ambavyo vitasambazwa kwenye hospitali za Halmashauri na vituo mbalimbali vya afya nchi nzima.

Rais Samia Suluhu Hassan azindua Ripoti ya Utafiti wa Afya ya Uzazi na Mtoto na Viashiria vya Malaria Tanzania 2022 na Ugawaji wa Magari ya kubebea Wagonjwa na Vifaa Tiba Jijini Dar es Salaam tarehe 28 Oktoba, 2023

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Wakuu wa Mikoa mara baada ya kuwasili kwenye ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam tarehe 28 Oktoba, 2023.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa na Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu, Waziri wa Afya (Zanzibar) Mhe. Nassor Mazrui, pamoja na Wakuu wa Mikoa wakati akikata utepe kuashiria uzinduzi wa magari ya kubebea Wagonjwa na Magari ya Usimamizi Shirikishi na Vifaa tiba kwenye hafla iliyofanyika kwenye ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam tarehe 28 Oktoba, 2023.
 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipiga makofi mara baada ya kuzindua magari ya kubebea Wagonjwa na Magari ya Usimamizi Shirikishi kwenye hafla iliyofanyika kwenye ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam tarehe 28 Oktoba, 2023.
 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza jambo mara baada ya kuzindua magari ya kubebea Wagonjwa na Magari ya Usimamizi Shirikishi kwenye hafla iliyofanyika kwenye ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam tarehe 28 Oktoba, 2023.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza jambo kabla kugawa Vifaa Tiba kwenye hafla iliyofanyika kwenye ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam tarehe 28 Oktoba, 2023.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Waziri Kindamba mfano wa Ufunguo kwa ajili ya Gari la Wagonjwa la Wilaya ya Handeni Mkoani Tanga kwenye hafla ya iliyofanyika kwenye ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam tarehe 28 Oktoba, 2023.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza jambo na Wakuu wa Mikoa mara baada ya kuzindua na kugawa magari ya kubebea Wagonjwa na Magari ya Usimamizi Shirikishi na Vifaa tiba kwenye hafla iliyofanyika kwenye ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam tarehe 28 Oktoba, 2023.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akikagua mabanda mbalimbali ya masuala ya Afya mara baada ya kuzindua magari ya kubebea Wagonjwa na vifaa tiba kwenye hafla iliyofanyika kwenye ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam tarehe 28 Oktoba, 2023.
 

Wadau wa Afya pamoja na Wageni mbalimbali waliohudhuria hafla ya uzinduzi wa Ripoti ya Utafiti wa Afya ya Uzazi na Mtoto na Viashiria vya Malaria Tanzania 2022, Ugawaji wa Magari ya kubebea Wagonjwa na Vifaa Tiba wakiwa kwenye ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam tarehe 28 Oktoba, 2023.