Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amemteua Mhifadhi William Simon Mwakilema kuwa Kamishna wa Uhifadhi wa Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA).
Kabla ya uteuzi huo, Mhifadhi Mwakilema alikuwa Naibu Kamishna wa Uhifadhi wa Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA).
Mhifadhi Mwakilema anachukua nafasi ya Dkt. Allan Herbert Kijazi ambaye ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.
Uteuzi huu umeanza tarehe 08 Januari, 2022.