TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

SALAMU ZA RAMBIRAMBI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan ametuma salamu za rambirambi kwa familia, ndugu, jamaa na marafiki kufuatia kifo cha aliyewahi kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) Mhe. Jecha Salim Jecha.

Kifo cha marehemu Jecha kimetokea tarehe 18 Julai, 2023 katika hospitali ya Lugalo jijini Dar es Salaam alipokuwa akipatiwa matibabu.

Rais Samia amepokea taarifa za kifo cha marehemu Jecha kwa majonzi na masikitiko makubwa.  

Vile vile, Rais Samia ametuma salamu za rambirambi kwa familia ya aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tatu Hayati Benjamin William Mkapa kufuatia kifo cha Bernard William Mkapa (Mwenye Mkuti) ambae alikuwa kaka yake.

Rais Samia amewaomba wanafamilia wote wawe na moyo wa uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha majonzi na amewaombea marehemu wote wapumzike mahali pema peponi, Amina.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *