Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwasili katika eneo la Bandari kwa ajili ya ukaguzi wa utendaji kazi wa Taasisi hiyo jijini Dar es Salaam.Katikati ni Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Mhandisi Deusdedit Kakoko.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa pamoja na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa pamoja Katibu Mkuu wa Sekta ya Uchukuzi Dkt. Leonard Chamriho wakitaza utendaji kazi wa mashine mbalimbali katika Bandari ya Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Mhandisi Deusdedit Kakoko akitoa maelezo kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kuhusiana na masuala mbalimbali ya utendaji kazi wa Mamlaka ya Bandari nchini.
Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Alphayo Kidata akitoa maelezo kuhusu utendaji kazi wa Taasisi yake inavyofanyakazi Bandarini huku Rais Dkt. Magufuli akimsikiliza.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akielekeza jambo wakati akikagua mtambo wa kukagulia mizigo ulioharibika kwa muda mrefu.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akielekea sehemu ya upakiaji na upakuaji wa mizigo katika eneo la Bandari jijini Dar es Salaam.
Rais Dkt. John Magufuli akisisitiza jambo mara baada ya kukagua eneo la upakuaji wa mizigo mbalimbali katika eneo la Bandari jijini Dar es Salaam.
Rais Dkt. John Magufuli akisisitiza jambo wakati akielekea eneo la Gati la upakuaji wa mafuta la kurasini KOJ katika Bandari ya Dar es Salaam.
Rais Dkt. John Magufuli akitoa maelekezo kwa Mhandisi Marry Mhayaya katika eneo la Gati la Mafuta la Kurasini KOJ
Rais Dkt. John Magufuli akiendelea na ukaguzi katika eneo la Gati la Mafuta la Kurasini KOJ.
Rais Dkt. John Magufuli akikagua utendaji kazi na vitendea kazi vya bandari katika eneo la ofisi ya mtambo wa kuhakiki mizigo katika eneo la Bandari jijini Dar es Salaam.