Daily Archives: July 20, 2015

RAIS KIKWETE AZINDUA MPANGO WA MODENAIZESHENI YA SEKTA YA MIFUGO JULAI 20,2015

unnamed

 

unnamed-1

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiweka saini kwenye jarida la Mpango wa Modenaizesheni ya Sekta ya Mifugo baada ya kuuzindua mpango huo leo Julai 20, 2015   

unnamed-2

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na maafisa waandamizi wa Wizara ya Mifugo baada ya kuzindua   Mpango wa Modenaizesheni  ya Sekta ya Mifugo Jumatatu Julai 20, 2015

unnamed-3

 

 

unnamed-4       Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na jamii ya wafugaji wa kabila la Kimaasai baada ya kuzindua  Mpango wa Modenaizesheni  ya Sekta ya Mifugo  Julai 20, 2015. Pamoja naye ni Waziri Mkuu wa zamani wa Kenya Mhe. Raila Odinga ambaye yupo nchini kwa ziara binafsi.

unnamed-5    Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisoma jarida la  Mpango wa Modenaizesheni  ya Sekta ya Mifugo leo Jumatatu Julai 20, 2015

unnamed-6     Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipena mikono na Dkt. Kaush Arha baada ya kuongea katika uzinduzi wa  Mpango wa Modenaizesheni  ya Sekta ya Mifugo  Julai 20, 2015. 

unnamed-7Rais Jakaya Mrisho Kikwete akizindua Mpango wa Modenaizesheni  ya Sekta ya Mifugo leo Jumatatu Julai 20, 2015

unnamed-8Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipatiwa maelezo kuhusu miradi ya maendeleo ya Wizara ya Mifugo kutoka kwa mmoja wa maafisa waandamizi wa wizara hiyo wakati  Mpango wa Modenaizesheni  ya Sekta ya Mifugo leo Jumatatu Julai 20, 2015. hata hivyo Rais alionesha kutofurahishwa na utendaji wa Wizara hiyo na kuwataka watendaji wake wabadilike kimawazo kwa kutenda kazi kwa njia za kisasa ili kuiendeleza sekta hiyo muhimu kwa haraka.

 

 

RAIS KIKWETE AREJEA NYUMBANI USIKU HUU JULY 18, 2015 BAADA YA KUKAMILISHA ZIARA YA KIKAZI YA USWISI

unnamed-1

kiwa Geneva, Rais Kikwete ameongoza vikao vya  Jopo la Kimataifa Linalopendekeza Jinsi Dunia inavyoweza kukabiliana na majanga yajayo ya magonjwa ya milipuko ambalo kazi yake imeungwa mkono na nchi 21 ambazo zilichangia mapambano dhidi ya ugonjwa wa Ebola.

Miongoni mwa mikutano ambayo Rais Kikwete ameiongoza katika Makao ya Umoja wa Mataifa (UN) mjini Geneva ni pamoja na yeye na wanajopo wenzake kutoa maelezo kuhusu maendeleo ya kazi yao kwa nchi ambazo zilichangia mapambano dhidi ya ugonjwa wa Ebola katika nchi za Guinea, Liberia na Sierra Leone.

Nchi hizo ambazo zimeunga mkono kazi ya Jopo hili katika mkutano huo ni Venezuela, Umoja wa Ulaya (EU), Uholanzi, Finland, Shirikisho la Russia (Russian Federation), Norway, China, Ubelgiji, India, Ujerumani, Marekani, Uswisi, Canada, Brazil, Denmark, Uingereza, Israel, Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), Umoja wa Afrika (AU), Benki ya Dunia (WB), Jamhuri ya Korea na Japan.

Pamoja na kwamba wajibu mkuu wa Jopo hili siyo kuchunguza ugonjwa wa Ebola na madhara yake, bado ugonjwa huo ni msingi mkuu wa kazi ya Jopo hilo ambalo wajibu wake ni kutumia uzoefu wa Ebola kutoa mapendekezo ya jinsi dunia inavyoweza kukabiliana na majanga ya magonjwa ya milipuko katika siku zijazo.

Ugonjwa wa Ebola ambao ulilipuka katika nchi hizo tatu za Afrika Magharibi mwishoni mwa mwaka 2013 mpaka sasa umeua watu 11,000 katika nchi hizo na kusababisha mshtuko mkubwa duniani.

Hiyo ilikuwa mara ya 24 kwa ugonjwa huo kulipuka katika Afrika tokea ulipolipuka kwa mara ya kwanza mwaka 1976, miaka karibu 40 iliyopita, katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) wakati huo ikiitwa Zaire.

Hata hivyo, katika milipuko ya kwanza 23, ugonjwa huo uliua watu wachache zaidi kuliko mlipuko wa 24.

Jopo hilo limeambiwa kuwa tofauti na matarajio ya dunia kuwa ugonjwa huo ulikuwa unamalizika katika nchi hizo hasa katika Liberia, umeanza kupata kasi tena na nchi hizo tatu zinakisiwa kuwa na wagonjwa karibu 70.

Jopo hilo lenye Wajumbe sita liliteuliwa Aprili, mwaka huu, na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Mheshimiwa Ban Ki Moon na kufanya vikao vyake vya mwanzo Mei, mwaka huu, katika makao makuu ya UN, mjini New York, Marekani.

Mbali na kukutana na nchi zilizochangia mapambano dhidi ya Ebola, Rais Kikwete na Jopo lake limepata nafasi ya kumsikiliza aliyekuwa Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani (WHO), Kanda ya Afrika, wakati ugonjwa huo unalipuka Dkt. Luis Gomes Sambo wa Angola ambaye aliwaeleza wajumbe historia ya ofisi ya kanda hiyo iliyoko mjini Brazzaville, Jamhuri ya Congo, katika kukabiliana na ugonjwa huo.

Aidha, Wajumbe wa Jopo wamemsikiliza Mkurugenzi mpya wa Kanda, Dkt. Matshidizo Rebecca Moeti ambaye amezungumza kwa njia ya mkutanomtandao (teleconference) kutoka mjini Brazzaville. Dkt. Moeti alianza kazi yake Januari Mosi, mwaka huu, 2015.

Vile vile, Wajumbe wa Jopo wamesikiliza jitihada za Jamhuri ya Rwanda kukabiliana na magonjwa ya mlipuko kupitia kwa Waziri wa Afya wa nchi hiyo, Agnes Binagwaho ambaye naye alizungumza kwa mkutanomtandao kutoka Kigali, Rwanda.

Nje ya vikao hivyo, Rais Kikwete alikutana na kufanya mazungumzo na Katibu Mkuu Mstaafu wa UN, Mheshimiwa Kofi Annan. Katika mkutano huo kwenye Hoteli ya Intercontinental, viongozi hao wawili wamezungumzia masuala mbali mbali ya kimataifa, ikiwamo hali ya Burundi.

Rais pia amekutana kwa mazungumzo na Mtendaji Mkuu wa Kituo cha South Centre ambacho kina makao yake mjini Geneva, Dkt. Martin Kohr. Kituo hicho kilianzishwa chini ya uongozi wa Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere, kwa nia ya utekelezaji wa Ripoti ya Kamisheni ya Nchi Zinazoendelea (South-South Commission), ambayo iliongozwa na Mwalimu.