Monthly Archives: May 2018

RAIS DKT.JOHN MAGUFULI ALIPOPOKEA RIPOTI YA UHAKIKI WA MALI ZA CCM, DKT.BASHIRU ALLY ATEULIWA KUWA KATIBU MKUU MPYA WA CCM.MEI 29,2018

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Dkt John Pombe Magufuli akiwa na Rais wa zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi na Makamu Mwenyekiti wa CCM (Visiwani) Dkt. Ali Mohamed Shein wakiwa na ‘mlima’ wa makabrasha ya ripoti ya uhakiki wa mali za chama baada ya kukabidhiwa na tume aliyounda kuchunguza mali hizo ukumbi wa Kikwete jijini Dar es salaam Mei 29, 2018.

Wa kwanza kushoto ni Dkt Bashiru Ali Kakurwa ni Mwenyekiti wa Tume iliyoundwa na  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Dkt John Pombe Magufuli kuchunguza na kuhakiki mali za CCM akiwa na wajumbe wa tume hiyo mara tu baada ya jina lake kupendekezwa kuchukua nafasi ya Katibu Mkuu wa CCM mbele ya wajumbe wa Mkutano wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya chama hicho ukumbi wa Kikwete jijini Dar es salaam Mei 29, 2018.

Wajumbe wa Mkutano wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya  CCM wakisamama na kuunga mkono kwa kauli moja pendekezo la Dkt. Bashiru Ali Kakurwa kuwa Katibu Mkuu mpya wa CCM ukumbi wa Kikwete jijini Dar es salaam Mei 29, 2018.

Mwenyekiti wa Tume iliyoundwa na  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Dkt John Pombe Magufuli kuchunguza na kuhakiki mali za CCM  Dkt. Bashiru Ali Kakurwa akipongezwa  na wajumbe wa tume hiyo mara tu baada ya jina lake kupendekezwa kuchukua nafasi ya Katibu Mkuu wa CCM mbele ya wajumbe wa Mkutano wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya chama hicho ukumbi wa Kikwete jijini Dar es salaam Mei 29, 2018.

RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA DKT. JOHN MAGUFULI AWAANDALIA FUTARI WAGENI MBALIMBALI IKULU JIJINI DAR ES SALAAM.MEI 28,2018.

 

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wageni mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi walioshiriki katika futari aliyowaandalia Ikulu jijini Dar es Salaam.Mei 28,2018.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiwa amekaa na Rais mstaafu wa awamu ya Tatu Benjamin Mkapa wa pili kutoka kulia, Rais mstaafu wa awamu ya pili Ali Hassan Mwinyi, Makamu wa Rais Mstaafu Dkt. Mohamed Gharib Bilal pamoja na viongozi mbalimbali walioshiriki Futari iliyoandaliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli Ikulu jijini Dar es Salaam.Mei 28,2018.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Rais wa Zanzibar Dkt. Ali Mohamed Shein pamoja na Mufti wa Tanzania Sheikh Aboubakary Zubery mara baada ya kufuturu Ikulu jijini Dar es Salaam. wa pili kutoka kulia ni Waziri wa Dini kutoka Saudia Arabia Dkt. Saleh Abdulaziz Alashek.Mei 28,2018.

Wageni mbalimbali wakiwemo viongozi wastaafu pia walishiriki katika futari hiyo.Mei 28,2018.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Rais mstaafu wa awamu ya pili Ali Hassan Mwinyi mara baada ya kufuru Ikulu jijini Dar es Salaam.Mei 28,2018.

Mufti wa Tanzania Sheikh Aboubakary Zubery akiwa na Rais wa Zanzibar Dkt. Ali Mohamed Shein mara baada ya kufuturu Ikulu jijini Dar es Salaam.Mei 28,2018.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Rais mstaafu wa awamu ya tatu Benjamin Mkapa mara baada ya kufuturu Ikulu jijini Dar es Salam.Mei 28,2018.

 

Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Aboubakary Zubeiry Ally akiswalisha viongozi na waalikwa mbalimbali swala ya Magharibi kabla ya futari iliyoandaliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli Ikulu jijini Dar es salaam.Mei 28, 2018

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimkaribisha kufuturu Waziri wa masuala ya Dini wa Saudia Arabia Dkt. Saleh Abdulaziz Alashek Ikulu jijini Dar es salaam .Mei 28, 2018

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwakaribisha wageni mbalimbali kuchukua futari aliyowaandalia Ikulu jijini Dar es salaam.Mei 28, 2018 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akijiunga na wageni mbalimbali kuchukua futari aliyowaandalia Ikulu jijini Dar es salaam.Mei 28, 2018 .

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Venance Mabeyo, Inspekta Jenerali wa Polisi Simon Sirro, Inspekta Jenerali wa Magereza Dkt. Juma Malewa na wageni wengine wakichukua futari iliyoandaliwa na  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli Ikulu jijini Dar es salaam. Mei 28, 2018.

Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa na Mama Janeth Magufuri, Mama Mary Majaliwa, Mama Anna Mkapa na Mama Khadija Mwinyi wakati wa  futari iliyoandaliwa na  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli Ikulu jijini Dar es salaam.Mei 28, 2018

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia jambo na  Waziri wa masuala ya Dini wa Saudia Arabia Dkt. Saleh Abdulaziz Alashek na Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Ndg. Philip Mangula kwenye futari aliyoandaa Ikulu jijini Dar es salaam.Mei 28, 2018