Monthly Archives: August 2014

RAIS KIKWETE AKUTANA NA WAJUMBE WA KITUO CHA DEMOKRASIA TANZANIA (TCD) IKULU NDOGO DODOMA AUGOSTI 31,2014

1

Mwenyekiti wa Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD) Mhe John Cheyo akiongea na Makamu Mwenyekiti wa TCD Mhe Philip Mangula, Katibu Mkuu wa CCM Ndg. ABdulrahman Kinana na Mhe Isack Cheyo walipowasili Ikulu ndogo mjini Dodoma kukutana na Rais Jakaya Mrisho Kikwete leo. Nyuma yao ni Mwenyekiti wa TLP Mhe Augustine Lyatonga Mrema na Mwenyekiti wa UPDP Mhe Fahmi Dovutwa leo.TCD inaundwa na vyama vyenye uwakilishi bungeni, ambavyo ni CCM, CUF, CHADEMA, TLP, NCCR-Mageuzi na UDP. 2

Mwenyekiti wa Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD) Mhe John Cheyo , Makamu Mwenyekiti wa TCD Mhe Philip Mangula, Katibu Mkuu wa CCM Ndg. Abdulrahman Kinana, Isack Cheyo, Mhe Augustine Lyatonga Mrema na Mhe Fahmi Dovutwa wakielekea chumba cha mikutano Ikulu Ndogo mjini Dodoma leo3

Wajumbe  wa TCD wakielekea chumba cha Mikutano4

Mwenyekiti wa NCCR-MAGEUZI Mhe Joseph Mbatia, Katibu Mkuu wa CHADEMA Dkt Wilbroad Slaa wakiwasili Ikulu Ndogo mjini Dodoma leo 5

Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi Mhe James Mbatia na Mwenyekiti wa CUF Profesa Ibrahim Lipumba na wakiwasili Ikulu ndogo mjini Dodoma leo6

Wajumbe wa TCD wakielekea chumba cha Mikutano Ikulu ndogo mjini Dodoma leo7

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana  na wajumbe wengine wa TCD alipokutana nao leo Ikulu Ndogo mjini Dodoma

 8

 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana  na wajumbe wengine wa TCD alipokutana nao leo Ikulu Ndogo mjini Dodoma 10

 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana  na wajumbe wengine wa TCD alipokutana nao leo Ikulu Ndogo mjini Dodoma 11

 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana  na wajumbe wengine wa TCD alipokutana nao leo Ikulu Ndogo mjini Dodoma 12

 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana  na wajumbe wengine wa TCD alipokutana nao leo Ikulu Ndogo mjini Dodoma 13

 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana  na wajumbe wengine wa TCD alipokutana nao leo Ikulu Ndogo mjini Dodoma 15

 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana  na wajumbe wengine wa TCD alipokutana nao leo Ikulu Ndogo mjini Dodoma 16

 Rais Kikwete akizungumza  na wajumbe wa Kituo cha Demokrasia Tanzania alipokutana nao Ikulu Ndogo Mjini Dodoma leo 17

 Rais Kikwete akizungumza  na wajumbe wa Kituo cha Demokrasia Tanzania alipokutana nao Ikulu Ndogo Mjini Dodoma leo18

  Rais Kikwete akizungumza  na wajumbe wa Kituo cha Demokrasia Tanzania alipokutana nao Ikulu Ndogo Mjini Dodoma leo19

 Rais Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Kituo cha Demokrasia Tanzania baada ya kukutana nao Ikulu Ndogo Mjini Dodoma leo20

 Rais Kikwete akiagana na wajumbe wa Kituo cha Demokrasia Tanzania baada ya kukutana nao Ikulu Ndogo Mjini Dodoma leo21

 Rais Kikwete akiagana na wajumbe wa Kituo cha Demokrasia Tanzania baada ya kukutana nao Ikulu Ndogo Mjini Dodoma leo22

Rais Kikwete akiagana na mjumbe wa Kituo cha Demokrasia Tanzania na Mwenyekiti wa TLP Mhe Augustune Lyatonga Mrema Ikulu Ndogo Mjini Dodoma leo. 

 

 

 

 

 

 

 

 

RAIS KIKWETE AZINDUA UJENZI WA DARAJA LA GULWE MPWAPWA AGOSTI 29,2014

JIWE LA MSINGI DARAJA LA GULWE-WILAYANI MPWAPWA.

Rais Jakaya Kikwete amesisitiza kuwa ujenzi wa daraja la Gulwe katika mto Sinyasungwi ni mwanzo wa ujenzi wa barabara ya Mbande-Kongwa-Mpwapwa-Kibakwe yenye urefu wa kilomita 101, kwa kiwango cha lami.Akiweka jiwe la msingi na kuzindua ujenzi wa daraja hilo lenye urefu wa mita 170 na uwezo wa kupitisha tani 150 rais kikwete amesema daraja hilo licha ya kuunganisha jimbo la Mpwapwa na Kibakwe pia litamaliza kero ya muda mrefu iliyokuwa ikiathiri barabara na reli katika eneo la Gulwe na Godegode wilayani Mpwapwa. “Kukamilika kwa daraja hili itakuwa jawabu la kudumu kwa reli na barabara katika eneo la Gulwe na hivyo kazi yenu sasa ni kutunza mazingira ili maji yafuate mkondo na hivyo kutoathiri miundombinu na mashamba ili kukuza shughuli za kilimo”,amesisitiza Rais Kikwete. Naye Waziri wa ujenzi Dkt. John Magufuli amezungumzia umuhimu wa halmashauri nchini ikiwemo ya Mpwapwa kutumia fedha za mfuko wa barabara kujenga barabara zake kwa kiwango cha lami ili kuboresha miundombinu ya miji na kuwataka wananchi kuacha kuchimba mchanga karibu na madaraja na barabara ili kulinda miundombinu hiyo na kuiwezesha kudumu kwa muda mrefu.Dkt. Magufuli amesema ujenzi wa barabara ya Mbande-Kongwa-Mpwapwa-Kibakwe hadi Chipogoro yenye urefu wa kilomita 120, utafanyika kwa awamu tatu ambazo ni Mbande-Kongwa-Mpwapwa, Mpwapwa-Kibakwe na Kibakwe-Chipogoro ili kuiunganisha barabara hiyo na ile ya tanzam na hivyo kuiunganisha wilaya ya Mpwapwa na kupunguza magari yaendayo Morogoro na Dare s salaam kupitia Dodoma.Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa barabara nchini (TANROADS), mhandisi Patrick Mfugale amesema ujenzi wa daraja la Gulwe lenye urefu wa mita 170 utahusisha ujenzi wa makalvati 9 yatakayosaidiana na daraja kupitisha maji na barabara ya kilomita 1.5 kila upande wa daraja na linatarajiwa kugharimu kiasi cha shilingi bilioni 3.3 litakapokamilika na litakuwa na uwezo wa kubeba tani 150 kwa wakati mmoja.1

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete wakwanza kushoto  akiwa na Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli, Mbunge wa Mpwapwa Mheshimiwa Gregory Teu pamoja na Mbunge wa Kibakwe ambaye pia ni Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mheshimiwa George Simbachawene, akiweka jiwe la msingi kama ishara ya kuzindua rasmi ujenzi wa Daraja la Mto Gulwe lenye urefu wa mita 170 litakalo unganisha kati ya Wilaya ya Mpwapwa na Kibakwe.2

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Askofu Mkuu wa Kanisa la Anglicana Tanzania Jacob Chimeleja, Waziri wa Ujenzi Dkt. John Pombe Magufuli, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Rehema Nchimbi, Mbunge wa Mpwapwa Mheshimiwa Gregory Teu, Mbunge wa Kibakwe ambaye pia ni Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mheshimiwa George Simbachawene pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Mhandisi Mussa Iyombe,  akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi ujenzi wa Daraja la Mto Gulwe lenye urefu wa mita 170.8

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete  akiwa na Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli wakiwa katika picha ya  pamoja na Mkandarasi,viongozi wa dini na kitaifa mara baada ya Rais kuzindua rasmi ujenzi wa daraja la Gulwe.9

 Daraja la Gulwe linalotumika sasa kama linavyoonekana hali iliyopelekea Serikali ya awamu ya nne kupitia Wizara ya Ujenzi kuanza kujenga daraja kubwa na la kisasa la Gulwe litakalokuwa na mita 170 mara baada ya kukamilika kwake.3

 Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia jambo wakati akipita mbele ya Mitambo itakayotumika katika ujenzi wa Daraja la Gulwe lenye urefu wa Mita 170.4

 Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli wapili kutoka kulia akiwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Mhandisi Mussa Iyombe wakwanza kulia, Mwenyekiti wa Bodi ya Usajili wa Wahandisi ERB Profesa Ninatubu Lema watatu kutoka kulia pamoja na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara Nchini TANROADS Mhandisi Patrick Mfugale wakifatilia ngoma za asili kabla ya uzinduzi rasmi wa Daraja la Gulwe5

 Ujenzi wa Makalvati yatakayosaidia Daraja kupitisha maji katika mto Gulwe kama yanavyoonekana. Jumla ya Makalvati tisa yatajengwa katika daraja hilo la mita 170.6

 Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimpokea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete ili kuweka jiwe la msingi kuashiria uzinduzi rasmi ujenzi wa Daraja la Gulwe lenye urefu wa mita 170.7

Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli (katikati) akizungumza na Mbunge wa zamani wa Mpwapwa George Malima Lubeleje kabla ya uzinduzi rasmi wa ujenzi wa Daraja la Gulwe lenye urefu wa mita 170.10

Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Mhandisi Mussa Iyombe wakwanza kulia akiwatambulisha Wakurugenzi, Wenyeviti, Wakuu wa Taasisi zilizochini ya Wizara ya Ujenzi kabla ya uzinduzi rasmi wa ujenzi wa Daraja la Gulwe litakalokuwa na mita 170.