Monthly Archives: February 2017

RAIS YOELI KAGUTA MUSEVENI AWASILI DAR ES SALAAM KWA ZIARA RASMI YA KISERIKALI YA SIKU MBILI FEBRUARI 25,2017

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimlaki Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni alipowasili  katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam kuanza ziara rasmi ya kiserikali ya siku mbili Februari 25, 2017

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimtabulisha kwa wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama  Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni alipowasili  katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam kuanza ziara rasmi ya kiserikali ya siku mbili  Februari 25, 2017

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni wakisimama kwa nyimbo za Taifa mgeni alipowasili  katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam kuanza ziara rasmi ya kiserikali ya siku mbili  Februari 25, 2017

Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni akikagua gwaride alipowasili  katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam kuanza ziara rasmi ya kiserikali ya siku mbili Februari 25, 2017

Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni akisalimiana na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan alipowasili  katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam kuanza ziara rasmi ya kiserikali ya siku mbili Februari 25, 2017

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akitambulishwa kwa ujumbe wa Uganda na  Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni alipowasili  katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam kuanza ziara rasmi ya kiserikali ya siku mbili  Februari 25, 2017Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni wakiangalia ngoma za utamaduni mgeni alipowasili  katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam kuanza ziara rasmi ya kiserikali ya siku mbili  Februari 25, 2017

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni  wakiwasili Ikulu jijini Dar es salaam tayari kuanza ziara rasmi ya kiserikali ya siku mbili  Februari 25, 2017

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia wakati mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni akipiga ngoma alipowasili Ikulu jijini Dar es salaam kuanza ziara rasmi ya kiserikali ya siku mbili Februari 25, 2017

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni alipowasili Ikulu  jijini Dar es salaam kuanza ziara rasmi ya kiserikali ya siku mbili Februari 25, 2017 

RAIS DKT.JOHN POMBE MAGUFULI FEBRUARI 23,2017 AMEMSAIDIA DADA NEEMA MWITA WAMBURA ALIYEMWAGIWA UJI WA MOTO NA MUMEWE MKOANI MARA.

Dada Neema Mwita Wambura (32) akizungunza na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kupitia njia ya Simu akimshukuru kwa msaada aliompatia wa kufanyiwa tena uchunguzi wa afya yake katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Pia Rais Dkt. Magufuli ameahidi kumpatia hifadhi mama huyo pamoja na watoto wake watatu ambao kwa sasa wapo Bunda mkoani Mara. Pia Rais Dkt. Magufuli alimpatia msaada Dada huyo kiasi cha Shilingi laki tano. Dada Neema Mwita Wambura aliungua vibaya mara baada ya kumwagiwa uji wa moto uliokuwa unachemka jikoni na mume wake katika kijiji cha Kyagata, Tarime mkoani Mara.

Mama Mjane Mariam Amir ( Bibi Mwaija ) ambaye amempa hifadhi Neema Mwita Wambura nyumbani kwake Tandika Davis Corner akiomba dua kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kupitia njia ya Simu kumshukuru mara baada ya kuzungumza naye kuhusiana na kumsaidia Dada Neema Mwita Wambura (32). Rais Dkt. Magufuli amempongeza Mama huyo Mjane ambaye ameonesha moyo wa kizalendo na kumpa hifadhi Dada huyo aliyemwagiwa uji wa moto na mumewe katika kijiji cha Kyagata, Tarime mkoani Mara. Pia Rais Dkt. Magufuli alimpa Mjane huyo kiasi cha Shilingi laki tano.

Dada Neema Mwita Wambura (32) wakwanza kulia akiwa pamoja na Mama Mjane Mariam Amir ( Bibi Mwaija ) wakiwa ndani ya gari mara baada Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kumsaidaia ili aweze kufanyiwa tena uchunguzi wa afya yake katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es Salaam.

 

Wauguzi wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili wakimpokea Dada Neema Mwita Wambura (32) na kuanza mara moja kumfanyia tena uchunguzi wa afya yake katika majeraha aliyoyapata mara baada ya kumwagiwa uji wa moto uliokuwa ukichemka jikoni kitendo kilichofanywa na mume wake.

Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili Profesa Lawrence Museru akimjulia hali Dada Neema Mwita Wambura (32) mara baada ya kufikishwa tena hospitalini hapo. Dada Neema Mwita alifanyiwa upasuaji mara nne katika siku za nyuma hospitalini hapo Muhimbili ili kutibu majeraha yake hayo ya moto.

Daktari Bingwa wa magonjwa ya dharura na Ajali katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili Dkt. Juma Mfinanga akizungumza kuhusu hali ya mgonjwa Dada Neema Mwita Wambura (32) aliyefikishwa tena katika Hospitalini hapo kwa ajili ya uchunguzi wa Afya yake.

Daktari Bingwa wa upasuaji wa ngozi kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili Dkt. Ibrahim Mkoma akizungumzia historia ya mgonjwa huyo ambaye yeye pamoja na jopo la madaktari bingwa walimfanyia upasuaji ili kutibu majeraha yake ya ngozi katika kipindi cha nyuma