Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimthibitisha Bw. James Wilbert Kaji kuwa Kamishna Generali wa Mamlaka ya udhibiti wa Dawa za kulevya nchini (DCEA), kabla ya kuapishwa Kamishina Jenerali James Kaji alikua akikaimu nafasi hiyo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli aki ongea baada ya kuwaapisha viongozi mbalimbali alio waapisha ikulu ya chamwino leo.
Kutoka kushoto Katibu Tawala wa mkoa wa Simiyu ,Mariam Perla Mmbaga, Mkuu wa mkoa wa Tabora Mhe. Dkt. Philemon Rugumiliza Sengati na CP, Thobias Emir Andengenye mkuu wa mkoa wa Kigoma wakila kiapo cha maadili baada ya kuapishwa mapema leo.
Wakuu wa wilaya wateule wakila kiapo cha maadili baada ya kuapishwa na Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli mapema leo julai 06-2020
Bi. Mariam Perla Mmbaga akiapa mbele ya Mhe. Rais Dkt. J.P.Magufuli Kuwa Katibu Tawala wa mkoa wa Simiyu hafla iliofanyika ikulu ya Chamwino Dodoma julai 06 – 2020
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha CP wa Polisi Thobias Emir Andengenye kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kigoma kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino Dodoma Julai 6, 2020
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akishuhudia Mkuu wa Morogoro Mhe. Loatha Ole Sanare akimuapisha Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza (SACP) Ismail Twahir Mlawa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Biharamulo kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino Dodoma Julai 6, 2020.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuliakishuhudia Mkuu wa Mkoa wa Pwani akimuapisha Mhandisi Martine Ntemo kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kibaha kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino Dodoma Julai 6, 2020
Wateuliwa wakila kiapo cha maadili ya Viongozi mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino Dodoma Julai 6, 2020
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea na watumishi na viongozi mbalimbali baada ya hafla ya uapisho wa viongozi mbalimbali aliowateua kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino Dodoma Julai 6, 2020
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiondoka baada ya kumalizika kwa hafla ya kuwaapisha viongozi mbalimbali alio waapisha ikulu ya chamwino julai 06-2020.