Monthly Archives: September 2015

RAIS DKT. JAKAYA MRISHO KIKWETE KATIKA MATUKIO MBALIMBALI YA PICHA UMOJA WA MATAIFA SEPTEMBA 29,2015

 

unnamedRais wa Jamhuri ya Muungano  wa Tanzania Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete jana jumanne amelihutubia kwa mara ya  mwisho Baraza Kuu la 70 la Umoja wa Mtaifa  akiwa Rais wa  Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.  Hotuba ya Mhe. Rais na ambayo iligusia mambo mengi ya kisiasa, kiuchumi, na  maendeleo  akitumia  pia fursa hiyo kuwaanga viongozi wenzie na kuwashukuru kwa ushirikiano waliompatia katika kipindi  cha  miaka kumi ya  uongozi wake,  iliwasisimua wajumbe  wa mkutano huo kiasi cha kukatishwa mara kwa mara kwa  makofi.

 Zifuatazo ni  baadhi ya picha  zinazomwonyesha Mhe.  Rais katika Matukio mbalimbali  Moja wapo Zikiwa ni  hafla  ambayo Rais wa Marekani, Mhe  Barack Obama aliiandaa kwaajili wa Viongozi Wakuu wa Nchi na  Serikali  waliohudhuria Mkutano wa 70 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa. 

Picha kwa hisani ya Uwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa

unnamed.0jpgRais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na   Mhe.Barack Obama na Mkewe  Michelle  Obama wakati wa hafla  ilioandaliwa na  Rais wa Marekani kwaajii ya   Viongozi wa Wakuu  Nchi na Serikali wanaohudhuria Mkutano wa 70 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa 

unnamed-1Mhe. Rais Kikwete akiwa na  Mhe. Sophia Simba, Katibu Mkuu  Balozi  Liberata Mulamula na mwanamitindo  Flaviana Matata muda mfupi mara baada ya kulihutubia  Baraza Kuu la  70 la Umoja wa Mataifa

unnamed-2Mwakilishi wa Kudumu wa  Antigua na Bermuda  Balozi  Walton Alfonso Webson ambaye ni  mlemavu wa kutoona   akimwongoza Mhe. Rais Kikwete kwenda kuonana na   Waziri Mkuu wake, Mhe. Gaston Alphoso Browne aliyekuwa na mazungumzo wa Mhe.Rais mara baada ya Mhe. Rais kulihutubia  Baraza  Kuu la 70 la Umoja wa Mataifa.

unnamed-3

Mhe. Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika mazungumzo na  Waziri Mkuu wa Antigua na Barbuda Mhe. Gaston Alphonso Browne,  wengine katika mazungumzo hayo ni Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa,  Balozi Tuvako  Manongi,  Mwakilishi wa kudumu wa Antigua na Barbuda, Balozi Walton  Webson mwenye miwani myeusi na Mkurungezi wa  Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa Balozi  Celestin Mushy